Wakati wa utawala wa ukoloni barani Afrika, maelfu ya vinyago viliharibiwa. Nchi za Afrika zinataka virudi na makavazi makubwa zaidi kote ulaya yamekubali kutoa vinyago maarufu vya shaba vya Benin kwa mkopo kwenda Nigeria.
Sasa Ufaransa inazindua ripoti ya kutoa wito wa kutaka maelfu vinyango kutoka Afrika vilivyo kwenye makavazi yake kurudishwa Afrika.
Shaba za Benin
A brass plaque under the Benin Bronzes collectionHaki miliki ya pichaBRITISH MUSEUM
Image captionKinyago cha shaba kutoka Benin
Shaba za Benin ni mkusanyiko wa vinyago vya thamani kubwa vilivyokuwa kwenye kasri la kifalme la Oba, Ovonramwen Nogbaisi, katika ufalme wa Benin.
Vilichongwa kutoka kwa pembe za ndovu, shaba na kutoka kwa miti.
Vingi vilichongwa kwa madhabahu ya wafalme za zamani na malkia.
Mwaka 1897 Waingereza waliendesha uvamizi dhidi ya Benin kujibu shambulizi dhidi ya wanadiplomasia wa Uingereza.
Kando na vinyago vya shaba, vifaa vingi vilichukuliwa na sasa vinasambazwa kote duniani.
A picture shows two artefacts from the Benin Bronzes collection, a long-beaked bird and the monarch's bell, returned to the Benin kingdom by a British pensioner during a ceremony in Benin City, Nigeria, on June 20, 2014.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionVinyago hivi vya shaba kutoka Benin vilirudishwa Nigeria mwaka 2014 kutoka Uingereza.
Makavazi mjini London yanasema kuwa vifaa kutoka Benin viliwasilishwa kwake mwaka 1898 na ofisi ya mashauri ya nchi za kigeni.
Mwezi Oktoba makavazi makubwa ya barani Ulya yalikubali kutoa kwa mkopo vinyago kwenda nchini Nigeria kwa makavazi yake mapya yanayopangwa kufuguliwa mwaka 2021.

Simba wala watu

Sanamu ya simba wawili kutoka Tsavo zilinyakuliwa na kupelekwa Chicago, IllinoisHaki miliki ya pichaFIELD MUSEUM OF NATURAL HISTORY
Image captionSanamu ya simba wawili kutoka Tsavo zilinyakuliwa na kupelekwa Chicago, Illinois
Hawa ni simba wawili maarufu wala watu kutoka eneo la Tsavo nchini Kenya, Afrika Mashariki ambao waliwaua na na kuwala wafanyikazi wa reli kutoka nchini Uingereza waliokuwa na asili ya Kenya -Uganda mwishoni mwa karne ya 19 
Wafanyikazi hao walikuwa wakijenga reli kati ya Mombasa na ziwa Victoria kwa miezi tisa mnamo mwaka 1898.
Luteni kanali John PattersonHaki miliki ya pichaFIELD MUSEUM OF NATURAL HISTORY
Image captionLuteni kanali John Patterson mmoja wa simba aliyemuua
Simba hao walipigwa risasi na kuawa na mhandisi wa Ungereza Luteni kanali John Patterson.
Sanamu ya simba hao ilinunuliwa kutoka kwa Patterson na makavazi ya historia ya Marekani iliyopo mji wa mwaka 1925 na kuhifadhiwa kama vituo asilia vya kudumu.
Luteni kanali Patterson aliripoti kuwa simba hao waliwaua na kuwala takribani wafanyikazi 135 wakiwemo waafrika weusi, Lakini makavazi inayohifadhi mabaki yao baadaye ilisema watu waliouawa walikuwa karibu 35.
Hayo ni kwa mujibu wa utafiti wa wanasayansi wao.
Makavazi ya kitaifa ya Kenya sasa inataka mabaki ya simba hao kurejeshwa nyumbani.
Jiwe la Rosetta
Jiwe la Rosetta katika makavazi ya Ungereza ya Bloomsbury Oktoba October 14, 2016 mjini LondonHaki miliki ya pichaAFP
Image captionJiwe la Rosetta katika makavazi ya Ungereza ya Bloomsbury Oktoba October 14, 2016 mjini London
Jiwe hilo la Rosetta la urefu wa mita 1.12 kwenye makavazi ya Uingereza likitokea nchini Misri.
Ni sehemu ya jiwe kubwa lenye maandishi juu yake ambayo yamewasaidia watafiti kujifunza jinsi kusoma kuhusu mifumo ya kuandika nchini Misri uliotumia picha na ishara.
Haijulikani vile jiwe hilo liligunduliwa mwezi Julai mwaka 1799 lakini kuna imani kuwa liliguduliwa na wanajeshi waliopigana na kiongozi wa jeshi la Ufaransa Napoleone Bonaparte wakati wakijenga kwenye mji wa Rashid.
Wakati wa Napoleon, Waingereza walichukua umiliki wa jiwe hilo chini ya makubaliano yaliyofahamika kama Treaty of Alexandria mwaka 1801.
Malkia Bangwa
Mchongo wa malkia Bangwa Queen kwa sasa unamilikiwa na wakfu wa Dapper mjini Paris, UfaransaHaki miliki ya pichaDAPPER FOUNDATION
Image captionMchongo wa malkia Bangwa Queen kwa sasa unamilikiwa na wakfu wa Dapper mjini Paris, Ufaransa
Hii ni sanamu maarufu la kuchongwa la Malkia Bagwa kutoka inayojulikana sasa kama Cameroon mwishoni mwa karne ya 19.
Sanamu hilo lenye urefu wa inchi 32 au (sentimita 81) linaashiria madaraka na afya ya watu wa Bangwatall Bangwa.
Ni moja ya sanamu maarufu zaidi Afrika na ina umuhimu mkubwa kwa watu nchini Cameroon.
Sanamu zilichongwa na kupewa majina ya wake wa wafalme au wanaufalme na kuitwa Malkia wa Bangwa huko Bangwa.
Sanamu ya Malkia wa Bangwa labda ilipewa au kuibwa na wakoloni wa Ujerumani karibu mwaka 1899 kabla ya eneo hilo kutawaliwa na wakoloni.
Vito vya thamani vya Maqdala
V&A Museum, Maqdala 1868 display: Crown, gold and gilded copper with glass beads, pigment and fabric, made in Ethiopia, 1600-1850Haki miliki ya pichaV&A MUSEUM
Image captionTaji la Maqdala
Vito vya thamani ya Maqdala ni pamoja na taji la karne ya 18 na nguo ya harusi vilivyochukuliwa kutoka Ethiopia na jeshi la Uingereza mwaka 1868.
Wanahistoria wanasema ndovu 15 walihitajika kubeba vifaa vilivyoibwa kutoka Maqdala.
Waingereza walivamia Maqdala kupignha kutwalia kwa ubalozoi wao wakati uhusiano kati ya pande hizo ulidorora.
V&A Museum, Maqdala 1868 display: Cotton dress embroidered with silk, said to have belonged to Queen Woyzaro Terunesh, made in the 1860sHaki miliki ya pichaV&A MUSEUM
Image captionNguo hii ya miaka ya 1860 inaaminiwa kuwa ya malkia Woyzaro Terunesh
Ndege wa Zimbabwe
The Zimbabwe BirdHaki miliki ya pichaWIKICOMMONS
Image captionNdege wa Zimbabwe
Vinyago nane wa ndege wa Zimbabwe waliibwa kutoka mahame ya mji wa zamani.
Ni ndege nane waligunduliwa. Walikuwa kwennye kuta za mji wa kale uliojengwa kati ya karne ya 12 na 15 na wahenga wa watu wa Shona.
Saba kati ya vinyago hao walikuwa nchini Zimbabwe tangu mwaka 2003 wakati mmoja alirudishwa kutoka Ujerumani.