HISTORIA YA WABENA
ASILI YA KABILA LA WABENA
Kwa sasa Wabena ni moja ya kabila linalopatikana katika mkoa wa Iringa na Njombe. Ni moja ya kabila ambalo lugha yake ina utajiri wa maneno, lugha hiyo inaitwa kibena.
Historia inafahamika kuwa makabila mengi ya kibantu hapo mwanzoni hayakuwa katika makundi ambayo yaliwatambulish
Wabena ni moja ya kabila ambalo lilijiwekea historia kubwa hasa pale kwenye vita kati ya Wakamba na Wazaramo kwenye miaka ya 1750. Mwanzoni kabisa kabila hili halikufahamika kama Wabena. Wabena walipata kuishi wakiwa na mahusiano mazuri na kabila la Wazaramo.
Historia ya Wabena inafafanuliwa kwa ufupi kuwa, kabla ya kabila hili kuwa katika ngazi ya kabila lilikuwa katika ngazi ya ukoo. Ukoo huo uliitwa Wang’hoo. Na ukoo huu ulipata kujulikana na Wazaramo na uli pendwa sana. Ukoo huu ulikuwa ukijihusisha sana na biashara zilizokuwa zikifanywa maeneo ya mwambao ambapo Washomvi walikuwa wenyejii.
Kulitokea wakati kuliingia watu kutoka katika ardhi ya Ukamba yaani Wakamba. Watu hao walivamia maeneo ya pwana na kufanya vurugu kwa Wazaramo na wenyeji wengine waliokuwa wakiishi kwenye maeneo hayo. Wakati huo Wakamba wakiingia kwenye ardhi ya Wazaramo, kulikuwa na Shujaa wa kizaramo aliyejulikana kwa jina la Bwana Pazi Kilama aliyekuwa akiishi maeneo ya Kinyangulu.
Kutokana na vurugu hizo zilizokuwa zikifanywa na Wakamba, baadhi ya wenyeji pamoja na Wafanyabiashara
Miongoni mwa wanajeshi walitoka kwenye ukoo wa Wang’hoo. Na kutokana na uhimara wao, walipigana kwa nguvu zote na kuwapiga Wakamba wote na kuwafukuza. Na mara baada ya vita kuisha, inasemekana kuwa Wang’hoo waliamua kuwa wakishinda vita watavunja silaha zao zote na kutafuta zingine kama tuu pakitokea vita nyingine.
Kitendo kile kilimshangaza sana Pazi Kilama. Na alishtuka sana kuona ukoo ule ukifanya tukio hilo la ajabu sana. Na kutokana na hiyo, ndipo pazi alipoamua kusema kuwa:
"kuanzia leo hamtaitwa Wang’hoo, na jina lenu litakuwa Wabena migoha. Ambapo kwa lugha ya kizaramo kubena maana yake ni kuvunja na migoha ni mikuku".
Na alifanya hivi kwa lengo la kutunza kumbukumbu, kwani kila vita bwana Pazi alikuwa akiweka historia kwa lengo la Watu kuja kujifunza. Hivyo pazi aliamua kuwaita Wabena Migoha. Na kutokana na mahusiano mazuri Wabena walipata kuishi na kushirikiana na Wazaramo, walizaliana na kuongezeka na walitawanyika sehemu mbalimbali kutokana na shughuli zao.
Na mpaka Wazungu wanafika katika ardhi ya Tanzania kwenye miaka ya 1850, walikuta kabila linalojitoshele
Hii ndiyo asili ya jina Wabena. Bado historia hii ni ndogo sana hivyo ni wakati wa kila mtanzania kuikuza historia ya kabila hili.
— with Mariam S Nyagawa, Herieth Man Utd, Renatus Mhada, Nesmelk Njawike and Mkomi Malemba
0 Comments