Image result for kabila la wasara

1. 2016 | KABILA LA WASARA NA TAMADUNI ZAO ZENYE KUHUSIANA NA UTUMWA
2. UTANGULIZI NA UCHAMBUZI WA HISTORIA NA TAMADUNI ZA KABILA LA WASARA Bara la Afrika ni moja la bara ambalo lina historia ndefu sana. Historia ambayo iljengwa na Waafrika wenyewe na zingine zilijengwa na watu ambao sio waafrika lakini wakishirikiana na Waafrika .Kwa upande mwingine kuna tamaduni ambazo zilianzishwa na waafrika wenyewe ili kukabiri mazingira yao na zipo tamaduni zingine ambazo Waafrika walizianzisha kutokana na ujio wa wageni. Miongoni mwa makabila ambayo tamaduni zao zimletwa kutokana na ujio wa wageni mfano mzuri ni Wamakonde kutoka kusini mwa Tanzania na Wasara au Wakeeni kutoka kusini mwa nchi ya Chad. Makala hii fupi tutaangalia kabila la Wasara na utamaduni wao wa kujichora usoni na kutoboa midomo wenye kuhusiana na baishara ya utumwa.Lakini ukweli ni kwamba kabila hili halikuandika chochote juu ya historia yao, hivyo ilikuwa kazi kwa wanakiolojia kufanya utafiti. Wanaakiolojia walifanikiwa kuvumbua vitu vingi vilivyosaidia kufahamu historia ya kabila la Wasara. Kwa mfano, mabaki ya nyumba, michoro, vyungu, vifaa vya chuma, mawe na vyombo mbalimbali ambavyo vilifanyiwa utafiti wa akiolojia. Wasara au wakareeni ni moja ya kabila linalopatikana katika familia lugha ya Nilo-Saharani. Lugha wanayoongea inaitwa Bongo-Bagirmi .Wanapatikana kusini mwa nchi ya Chad na wachache wanapatikana katika nchi ya Afrika ya kati. Ni miongoni mwa makabila ambayo tamaduni zao zinauhusiano mkubwa na biashara ya utumwa ilikuwa ikihusisha kuvuka jangwa la Sahara. Wasara ni miongoni mwa makabila ambayo kwa sasa tamadunin zao zinapotea kutokana na tamaduni hizo kuhusishwa na masuala ya utumwa. Yaani kama vile historia ya kujichonga meno, kuchanja chale na kutoboa Ndonya kwa kabila la wamakonde wanaopatikana kusini mwa Tanzania.Kabila hili la Wasara lina mganyiko ambao unatokana na utofauti wa kijiografia, kisiasa na wakati mwingine hata kiukoo. Asili ya neno Sara linausiana sana na Watu wa Misri juu y a uwepo wa Mungu Jua. Neno hili ni la kiarabu lenye maana ya watoto wa Ra, Ra alikuwa mungu jua wa watu wa Misri. Asili ya jamii hii ya Wasara ilianzia huko Afrika ya kaskazini katika maeneo yalifahamika kama mto Chari na ziwa Chad. Wakazi wa mwanzo wa jamii hizi walifahamika kama Wasao ambao waliishi maeneo hayo takribani karne ya 6 kabla ya kristo kuzaliwa. Kwenye miaka ya 900-1000 miji ya wakazi ya Wasao ilikuwa imeendelea kwa kiasi kikubwa.Kama ilivyokuwa kwa Wabantu, pia Wasao waliweza kuhama kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe na uvamizi wa Waarabu. Hivyo wakagawanyika wapo waliobaki hapo na wengine walienda Kaskazini mashariki mwa mto Nile.Kutokana na kuhama huko nchi ya
3. wakazi wa Wasao ikaanguka na ndio ukawa mwisho wa jamii za Waso na kukawa na jamii ya Wasara mara baada ya kuchangamana na Watu wa Misri. Kwenye karne ya 9 na ya 10 biashara ya utumwa ilikuwa imeshamiri kaskazini mwa bara la Afrika. Miongoni mwa makabila yaliyoathiliwa sana kiutamaduni ni Wasara. Utamaduni wa kujichora usoni na kutoboa midomo kabla ya utumwa haukuwepo, ila tamaduni hizi zilikuja kuwepo mara baada ya biashara ya utumwa kushamiri. Kwa kawaida hakuna mtumwa aliyependa kuwa mtumwa, bali watu walikuwa wakilazimishwa kuwa watumwa.Hivyo kwa jamii za Waafrika suala la utumwa lilipingwa sana.Baishara ya utumwa ilihitaji watu waliokamilika kimaumbile na kimuonekano, yaani mtumwa hakupaswa kuwa na jeraha wala michubuko. Hivyo jamii za Wasara waliamua kujichora usoni na kutoboa midomo kwa kutumia kisu cha moto kwa ajili ya kujiweka alama, ili waarabu wakija wasiwachukue utumwani, kwani alama hizo zilikuwa kama vidonda. Hivyo kila mwanajamii alipaswa kufanya hivyo, kwani asipofanya hivyo atachukuliwa utumwa. Hivyo ikawa hivyo vizazi hadi vizazi na ikarithisha kama sehemu ya utamaduni. Na kwa wakati huo asijichora aliitwa mtumwa na alitengwa na jamii(historia hii inafanana na ile ya wamakonde). Ukweli ni kwamba uchorwaji wa michoro hiyo usoni na utoboaji wa midomo ilikuwa na maumivu makubwa sana, ilichukua wiki 2 hadi 3 kwa mtu kupona maumivu hayo.Kwa sasa utamaduni huu unaonekana kupitwa na wakati. Mfumo wa ndoa wa jamii ya Wasara upo tofauti kidogo na jamii zingine za kiafrika. Kulingana na mila na desturi za wasara, mume anapaswa kutoa mtama kwa familia ya mke ili apate kuoa. Ndoa za mitaala zilikuwepo. Na kwa upande mwingine taraka zilihusikla kwa kiasi kikubwa. Dini na imani kwa jamii za Wasara ilikuwa kama ifuatavyo, kipindi kabla ya ujio wa waislamu wasara walaiabudu miungu yao ya Jua. Na mara kipindi cha waislamu wapo walikuw waislamu na wapo walioendelea kuwa na imani zao zingine. Na mwisho kipindi cha ukoloni wapo waliokuwa wakristo na wengine wakiwa waislamu na dini zingine za jadi.
4. Kutoka mto Nile hadi kusini mwa nchi ya Chad, Mwanzoni jamii ya watu wa Sara walikuwa wakiishi maeneo ya kaskazini mashariki mwa mto Nile. Na kutokana na baishara ya utumwa kushamiri ilikuwa ikifanywa na waarabu, wasara wakaamua kukimbia na kufika maeneo ya kusini mwa nchi ya Chad. Lakini kwa upande wa kustaharabika jamii hizi zilistaharabika wakiwa kaskazini mashariki mwa mto Nile. Katika nchi ya Chad jamii hizi zinapatikana katika maeneo kama Moyen-Chari, Logone Oriental, Logone Occidental, na sehemu kubwa na mkoa wa Tandjile. Walifika maeneo haya wakitokea mto nile kwenye miaka ya 500 sawa na karne ya sita wakati huo Uislamu ulikuwa unaenea maeneo ya kaskazini mwa bara la afrika. Mpaka wakoloni ambao ni Wafaransa waliwaitwa Wasara watu ambao ni wazuri kutokana na muonekano wao. Na zaidi ni moja ya Waafrika ambao walienda kwa wingi kwenye vita zote za Dunia . Mpaka nchi ya Chad inapata uhuru kwenye miaka ya 1960, raisi wa kwanza alifahamika kwa jina la François Tombalbaye ambaye alikuwa anatoka kabila la Wasara. Wakati wa utawala wa mwana Francois Tombalbaye kulikuwa na migogoro ya hapa na pale kuwa nchi hiyo ilikuwa ilkiongozwa kwa misingi ya kikabila la Wasara. Migogoro itajadiliwa katiukan kipengere cha migogoro katika historia ya Wasara. Sanaa katika jamii za Wasara ni moja ya vitu muhumu sana, jamii za Wasara muda mwingi wa mapumziko wanaimba na kucheza nyimbo zao za asili. Na wakati mwingine uchongaji wa vinyago na uchoraji ni moja ya sanaa wanazofanya watu wa jamii ya Wasara. Madawa na magonjwa, kwa maisha ya jamii ya Wasara pia ni sehemu ya maisha yao ya kila siku kuanzia hapo mwanzo mpaka wakati huu. Kwa mujibu wa jamii hizo suala la kuumwa linachukuliwa kiimani zaidi, yaani kuumwa na kutokuumwa ni mipango ya Mungu. Na matambiko na sara ni moja ya njia ya kuponya ugonjwa huo.Hivyo suala la mtu kuumwa kwa jamii ya Wasara halina uhusiano na sayansi, yaani kwa mfano kumpeleka mtu hospitali au kuwa malaria inaambukizwa na mbu.
5. Suala la kifo na maisha baada ya kifo, pia ni miongoni mwa vitu ambavyo ni sehemu ya maisha kwa jamii ya Wasara.Ukweli ni kwamba kila jamii ya kiafrika inatazama suala la kifo na maisha baada ya kifo kwa mitazamo mbalimbali. Kwa mfano waliowaumini wa dini ya ukristo na uislamu wanaamini kuwa, wenye dhambi wataenda motoni na wasio na dhambi watakwenda mbinguni. Lakini kwa upande wa kabila la Wasara, dhana ya kifo na maisha baada ya kifo ni kwamba, suala la mtu kufa sio la kibaiolojia kama vile jamii zingine zinavyodhani. Kwao wanaamini kuwa kila binadamu ana roho na pindi kifo kikitokea roho inatengana na mwili.Kwa kuwa maisha ya Wasara walikuwa na mungu wao wa Jua mwenye asili yake huko Misri, basi waliamini kuwa Roho au marehemu anapofariki anaenda kuishi maisha mapya, na mtu alipaswa kuzikwa sehemu za wazi ili mungu Jua aweze kumuona marehemu huyo. Hivyo kwa kuwa marehemu alikuwa ni moja sehemu ya jamii, jamii ilipaswa kufanya sherehe ili kumtakia safari njema na maisha mapya huko aendako. Sherehe na sikukuu kwa jamii ya Wasara, pia ni jambo muhimu, sherehe nyingi za kabila hili zilihusisha matambiko, mazishi na mwanzo na mwisho wa mafunzo ya kijadi, yaani Jando na Unyago.Kwa Wasara wanaume waliopata mafunzo waliitwa Ndo, na wasichna na viajana wadogo waliitwa Koy.kwa wakristo wanasheherekea sikukuu kama wakristo wengine dunia na hta kwa waislamu ni hivyo hivyo. Migorogoro, katika historia ya Wasara inagawanywa katika sehemu mbili yaani kuna mgogoro kabla ya ujio wa wakoloni. Mgogoro huu unahusu mkapigano kati ya Wasara na Waarabu juu ya kueneza dini ya kiislamu kwa jamii za Wasara. Vita kati ya Wasara vilisababishwa na kitendo cha Wasara kupinga kuwa waislamu pamoja na biashara ya utumwa. Na mgogoro mwingine ni mara baada ya uhuru ambapo kunabaadhi ya watu walihoji serikali juu ya masuala ya dini na tamaduni. Mgogoro huu ni juu ya serikali na baadhi ya wasomi waliojaribu kuhojihoji juu ya masuala ya nchi yao kwani asilimia kubwa watumishi walikuwa kutoka jamii ya watu wa Sara. Ndio maana kwenye maiaka ya 1966 kulitokea vita vya wenyewe kwa wenyewe. Lugha ya Wasara na mgawanyiko wake,kabila la Wasara wanaongea lugha ya bongo- bagirmi ambayo inatoka katika familia lugha ya Nilo-Sahara.Lugha hii ya kabila la Wasara inahusisha lugha nyingi za bongo-bagtirmi ambazo zinatumiaka sana kusini mwa nchi ya chad. Na zingine chache zinaongelewa kaskazini mwa nchi ya Chad na Afrika ya kati.Wakati mwingine lugha hiyo inafahamika kama moja ya lugha inayopatikana Sudani ya kati. Kulingana na wataalamu waliofanya tafiti juu ya lugha za Afrika kama vile Greenberge (1966) ambapo yeye aliona lugha hii ina mgawanyiko wake. Yaani lugha hii ina lahaja na kila moja ikiwa na
6. wazungumzaji wake. Kwa upande wa Tucker na Bryan (1966) wao wanachukulia kuwa lugha ya Wasara kuwa ni moja ya lahaja ambayo inaongelewa sehemu kubwa ya nchi ya Chad. Hivyo wao wanachukulia kuwa lugha hii uenda ilikuwa ni sehemu ya lugha za Afrika ya kati au kaskazini mashariki mwa mto Nile. Licha ya Bongo-bagirmi kuwa lugha kubwa kwa jamii ya Wasara, kuna lugha ya biashara iliotumiwa na kabila hilo. Lugha hiyo ilifahamika kama Ngambay au Sara Ngambay . Lugha hii ilitumika sana maeneo ya kusini mwa nchi ya Chad ikiwa na mazungumzaji zaidi ya million moja.Licha ya kwamba lugha ya Sar au Sara Madjingly ni lugha ya kibiashara inayotumika nchi nzima. Bado lugha ya Kibongo- B agirmi ilikuwa lugha ya kwanza.Kwa ujumla lugha hii ya Sara imegawanyika katika sehemu zifuatazo , kuna Sara magharibi, Ngambay, Laka, Sara ya kati (Doba) Bedjond, Bebote, Mango, Gor e Kabba, Sara mashariki Sar, Nar, Mbay, Ngam, Dagba, Gulay, na Horo Masuala ya umiliki mali na usuluhishi, katika kipindi cha kabla ya ukoloni hakukuwa na mahakama wala hakukuwa na mfumo wowote maalumu wa kuhukumu.Kwani migogogro ya kifamilia haikutatuliwa na wakubwa wa ukoo wala wakubwa wa kijiji.Kama kukitokea hali ya kutokuwa na amani, migogoro ilitatuliwa ndani familia au ndani ya ukoo na sio kiongozi wa kijiji au kiongozi wa ukoo ambaye sio wa ukoo wenye mgogoro.Yaani migogoro ilitatuliwa na wenyewe ndani ya ukoo au familia. Na wakati mwingine maombi yanafanyika kwa mtu alifariki kama alikuwa chanzo cha mgogoro. Kwa ukoo au familia ambayo kuna mtu alifariki mali zilirithiwa na watoto na mzazi(wa kike). Ndugu wengine hawakupaswa kuchukua mali yoyote bila kuhusishwa wahusika. Mfumo wa siasa wa kabila la Wasara, hapo mwanzoni mfumo wa siasa au uongozi ulikuwa ni kifarao. Na hii ilitokana na kwamba jamii hizi kwenye miaka ya 500 k.k, walikuwa wakiishi kaskzini mashariki mwa mto Nile. lakini baada ya baiashara ya utumwa kabila la Wasara walikimbilia kusini mwa Chad ambapo huko mfumo wa siasa ulibadilika na ukawa chini ya machifu. Na mpaka wakoloni wanafika Wasara walikuwa chini ya mfumo wa uchifu. Lakini mara baada ya uhuru mfumo wa siasa ukawa chini y serikali, huku machifu wakiwa na nafasi katika makabila yao. Hii ndiyo historia fupi juu ya kabila la Wasara au Wakeeni wanaopatikana kusini mwa nchi ya Chad.ukweli ni kwamba nyaraka nyingi zenye kuhusu historia za Waafrika zipo katika lugha ya kigeni. Hivyo ni wakati wetu kutafsiri na kuchambua nyaraka hizo kwa faida ya Waafrika na watanzania wwote. Huu ni wakati wa kujifunza jamii zetu za kiafrika na historia yai kwa faida ya vizazi vijavyo. TUJADILANE ILI TUJENGE HISTORIA YETU.